Ijumaa, Machi 02, 2018

Wanawake wenye ulemavu wa ngozi kuandika historia mpya kwa kupanda mlima Kilimanjaro.

 
Mwanaharakati wa haki za binadamu na mpigania mabadiliko Jane Waithera akishirikiana Na mshindi wa tuzo ya muandaaji wa filamu na mpandaji wa milima mbalimbali Elia Saikaly wameandaa mradi unaojulikana kama "climb for Albinism"(kwea kwa ajili ya ualbino) ambapo wanawake sita kutoka Afrika wamejipanga kukwea mlima Kilimanjaro wenye kilele kirefu zaidi kuliko yote barani Afrika.

Akiongea na waandishi wa habari jana jijini Dar es salaam muanzilishi wa programu hiyo Elia Saikaly amesema kuwa Mara nyingi watu wenye ualbino wanaonekana kama waathirika na kusema kuwa wana mpango wa kuvunja dhana hiyo kwa kufanya kitu ambacho hakijawahi kufanyika na kusistiza kuwa wataionyesha dunia kwamba licha ya changamoto nyingi zinazowakabili na kusema kuwa wanawake hao wana nguvu, wana uwezo na ni mfano wa kuigwa kwa wanawake wengine duniani.

Aidha kiongozi mwenza wa "climb for albinism" Jane Waithera amesema kuwa watakaposimama kweye kilele cha Afrika, timu nzima itatuma ujumbe madhubuti utakaosaidia kuelimisha jamii na kuondoa mitizamo hasi inayoeneza fikra mbaya kuhusu watu wenye ualbino.

Kwa upande wake kiongozi wa shirika la under the same sun Peter Ash linalotetea haki na usitawi wa watu wenye ualbino kwa kuelimisha jamii kuhusu ualbino , amesema kuwa wanaunga mkono shughuli hizo za kupanda mlima huku akisisitiza kuwa wana ndoto kwamba siku moja watu wenye ualbino watachukua nafasi yao inayostahili kwenye jamii na kwamba siku za ubaguzi dhidi ya watu wenye albino zitakuwa kumbukumbu iliyofifia na kusema kuwa upandaji wa mlima huu utaionesha duniani kwamba ndoto hii inaweza kutimia.

Pia Nodumo Ncomanzi ambaye ni moja kati ya wapanda milima kutoka Zimbabwe amesema kuwa kupanda mlima ni njia nzuri itakayoonesha na kuwakumbusha watu kwamba albino Wapo na wanajitegemea na wanawake wenye ualbino wanastahili kupewa fursa ya kukabiliana na kuzishinda changamoto mbalimbali zinazowakabili.

RC MAKONDA AFANIKISHA NDOTO YA AHMED ALBAITY






Ndoto na shauku ya kijana Ahmed Albaity alieteseka kwa zaidi ya Miaka 10 Kitandani kwa kushindwa kumudu gharama za matibabu leo imebadilika kuwa furaha baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda kumkabidhi  Tiketi za Ndege za watu Wanne kwaajili ya safari ya kwenda kupatiwa matibabu Nchini China kwenye Hospital ya Beijing Puhua International huku akijitolea pia kugharamia fedha za Matibabu na Malazi.

 Makonda alitoa ahadi kumsaidia Ahmed Albaity wakati wa Zoezi la Upimaji Afya Bure kwenye Meli ya Jeshi la China mwishoni mwa Mwaka Jana baada ya kugundulika Ahmed anahitaji Matibabu Maalum ambayo hayapatikani kokote kule duniani isipokuwa China, jambo lililomfanya RC Makonda kutokwa na Machozi na Kuhaidi Kumpeleka kwenye matibabu kwa gharama yoyote ile *Maumivu na Mateso* anayopitia kijana huyo.

Ahmed Albaity anasumbuliwa na tatizo la uti wa mgongo baada ya kuanguka na kuvunjika Shingo alipokuwa akiogelea ambapo kwa sindano moja pekee inagharimu Dollars 26,000/= sawa na shillingi million 52.

RC Makonda amesema Ahmed atasafiri Nchini China Siku ya Jumapili akiongozana na watu watatu wa kumsaidia kumuhudumia ambapo gharama zake ni zaidi ya Shilingi Million 100.

Aidha RC Makonda amesema Shauku yake ni kugusa maisha ya Mwananchi hata kama ni mmoja atakaekwenda mbele za Mungu na kusema Asante Mungu kwa kutupatia viongozi wetu, ifike mahali tumtumikie Mungu katika nafasi zetu, na katika hilo watu wote watakuwa Sawa na tutawahudumia bila kutarajia chochote kutoka kwao kama sehemu ya utumishi wetu ambapo amewashukuru watu wote waliomchangia na kufanikisha matibabu.

Hata hivyo RC Makonda ametoa wito kwa wananchi wa dini zote kumuombea Ahmed ili aweze kupona na kuendelea na shughuli za ujenzi wa Taifa.

Kwa upande wa Ahmed Albaity amemshukuru RC Makonda kwa moyo wa ukarimu aliouonyesha ambapo ameeleza kuwa ameishi kwa mateso muda mrefu kutokana na kukosa uwezo wa kumudu gharama za matibabu.

Aidha amesema alipokuwa akiomba watu wamchangie wapo waliokuwa wakimvunja moyo kwa kumwambia hawezi kupona lakini RC Makonda ameonyesha moyo wa kipekee.

Jumatano, Januari 10, 2018

Yanga Leo kukipiga na URA




KIKOSI cha Yanga, leo kitapambana na URA ya Uganda katika mchezo wa nusu fainali ya michuano ya Mapinduzi inayoendelea kutimua vumbi mjini Unguja huku kocha wa Simba akiwapa mbinu. Mechi hiyo inayotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa itafanyika kwenye Uwanja wa Amaan mjini Unguja.


Hata hivyo, Aliyekuwa Kocha Mkuu wa Simba, Mcameroon, Joseph Omog ambaye hivi karibuni alifungashiwa virago na klabu hiyo, ameitaka Yanga kuhakikisha inacheza kwa nidhamu kubwa na URA kama inataka kuibuka na ushindi.

Akizungumza kwa njia ya simu kutoka kwao Cameroon, Omog alisema, kuwa wachezaji wa URA wanacheza kwa nidhamu kubwa na kwa ushirikiano wa hali ya juu ndiyo maana katika michuano hiyo timu hiyo inaonekana kuwa ni ngumu.

Alisema wachezaji wa Simba walipoteza umakini katika mechi zao na kushindwa kuzitumia vizuri nafasi walizokuwa wakizipata jambo ambalo ndilo limesababisha washindwe kuibuka na ushindi katika michezo yake. Amesema kwenye mechi dhidi ya URA walipoteza umakini ndiyo maana walifungwa kirahisi.

“Nimesikitishwa na kitendo cha Simba kuondolewa katika michuano hiyo lakini kila mtu anapaswa kukubaliana na matokeo hayo na hivyo ndivyo mchezo wa soka ulivyo. “Wachezaji wa Simba walipoteza kidogo umakini katika mechi hiyo ambayo video yake nimeiona leo (jana) kupitia mtandao baada ya kutumiwa na rafiki yangu mmoja ndiyo maana walifungwa japokuwa walicheza vizuri.

“Kwa hiyo, Yanga wanatakiwa nao kuwa makini katika mechi hiyo, kila mchezaji aingie uwanjani kupambana na kuyafanya majukumu yake kwa ufanisi mkubwa kama kweli wanataka kuibuka na ushindi, nimewaona URA ni wazuri na wanacheza kwa akili sana. “Yanga watafanya kosa kama watawaachia nafasi ya kutawala mchezo huo,” alisema Omog ambaye mwaka jana aliongoza timu hiyo kutinga fainali ya michuano hiyo lakini ikifungwa na Azam FC

Baada ya Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Lowassa kumtembelea Rais Magufuli...Mbowe azungumza haya

Baada ya Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Edward Lowassa kumtembelea Rais John Magufuli Ikulu jijini Dar es Salaam na kufanya nae mazungumzo, Mwenyekiti wa Chama hicho, Freeman Mbowe amesema kuwa kile kilichosemwa na Lowassa  sio msimamo wa CHADEMA bali ni mawazo yake binafsi.

Akizungumza jana na Idhaa ya Kiswahili ya Shirika la Utangazaji BBC, Mbowe alisema wao kama Chama wamekuwa na utaratibu wa kutoa msimamo wao na kueleza kuwa kwa siku za hivi karibuni wamekuwa na malalamiko dhidi ya Rais na Serikali yake kuhusu kuminywa kwa Uhuru wa Bunge, Mahakama na kuminya Demokrasia.

" Tunaona jinsi ambavyo uhuru wa watu unaminywa, uhuru wa vyombo vya habari, wandishi, wanasiasa na wananchi kutekwa, kudorora kwa uchumi, unaanzaje kumuunga mkono Rais nafikiri muhusika aulizwe mwenyewe," alisema Mbowe.

Kuhusu kauli ya Lowassa kusifia ongezeko la ajira, Mbowe anasema hayupo tayari kujibu hoja hiyo lakini akaeleza namna ambavyo makampuni mengi yanafungwa hivi sasa, kundi kubwa la vijana wasio na ajira likiwa mitaani.

" Nisikitike tu kuwa sisi tuna tatizo kubwa sana la kumuuguza Lissu ambaye alipigwa na risasi, kweli anaweza kutoka kiongozi mkubwa na kumsifia Magufuli wakati tunauguza watu? 

"Msaidizi wangu Ben Saanane amepotea hadi leo, wabunge wetu wanafukuzwa bungeni hivyo niseme tu hakuna msimamo kama huo ndani ya Chama labda atafutwe muhusika mwenyewe aeleze," Alisema Mbowe.

Akizungumzia hama hama kwa wabunge na wanachama wa upinzani na kujiunga na CCM sambamba na tukio la jana  la Mjumbe wa Kamati kuu ya Chama hicho, Muslim Hassanal kujiunga na CCM , Mbowe alisema suala la wapinzani kuhamia CCM halijaanza leo na kwamba suala la kujenga upinzani ulio imara lazima lipitie hatua mbalimbali ili kufanya mchujo wa kubakia na watu wenye dhamira ya kweli

Jumatatu, Desemba 04, 2017


 MAMBO MATANO YA KUFANYA KUMFURAHISHA MPENZI WAKO!
Image result for muslim couples
Kama wewe uko katika mahusiano na unataka kuyafanya yakue, ni vyema ukayachukulia hatua baadhi ya mawazo yanayoweza kufanya penzi lenu kuwa imara, lenye furaha na kujenga uaminifu kati yenu. Haya hapa ni mamo matano muhimu ambayo unaweza kuyafanya ili kumfanya mpenzi wako awe na furaha wakati wote:
Msikilize.
Wanawake wanapenda sana kusikilizwa, na unapotenga muda wako kumsikiliza huwa anahisi unamjali sana na hupata furaha. Japo wanaume wengi hawapendi kusikiliza, lakini inabidi ujitahidi kuwa karibu na mpenzi wako na utenge muda mzuri wa kumsikiliza.
Mnunulie zawadi za aina mablimbali.
Kama umezoea kumpa mpenzi wako zawadi za aina moja, mfano kumnunulia kadi kila anaposheherekea siku yake ya kuzaliwa, basi yahitaji ubadilike. Jaribu kusikiliza baadhi ya tarifa anazozitoa kuhusu vitu anavyopendelea, na anavyopenda kupokea. Jaribu kupata msaada wa kujua anapendelea nini kutoka kwa rafiki zake. Kumpatia mpenzi wako vitu anavyovipendelea zaidi kutalihuisha penzi lenu na kulifanya lionekane jipya tena.
Jitahidi kuwa karibu na marafiki zake.
Kitu cha msingi kufanya kwa muda wote ambao umekuwa katika mahusiano na mpenzi wako, jaribu kuwazoea rafiki zake. Jitahidi kuwa kuwazoea wale watu wa karibu naye. Huhitaji kuwazoea marafiki zake wote. Hii itakusaidia kumjua mpenzi wako zaidi na kujenga urafiki wenu.
Penda na thamini vitu anavyovipenda.
Kama mpenzi wako anapendelea vitu ambavyo wewe huvipendi, jitahidi kumuonyesha kuwa unavifurahia. Siyo lazima uvipende lakini unaweza kumsifia pale anapovifanya. Kuheshimiana ni chachu ya mafanikio katika  mahusiano, hivyo kama wewe umekuwa ukichukulia kana kwamba maslahi yake ni madogo, ni wakati wa kuanza kuonyesha kuwa unathamini baadhi ya vitu anavyovipendelea. Hii itamfanya ajisikie kuwa anapendwa na itaimarisha penzi lenu.
Tumieni wakati mwingi pamoja.
Mnapokuwa katika mahusiano ni muhimu kutenga muda wa kuwa na mpenzi wako. Mfano siku za weekend hakikisha unamtembelea ama mnakwenda maeneo kama vile maktaba, mghahawani, kwenye bustani za mji, ufukweni na maeneo mengine mbalimbali ambayo hamjawahi kuyatembelea. hii itawajengea ujasiri na kuaminiana katika mahusiano yenu.

Jumatano, Novemba 22, 2017

Jinsi ya kutunza Upendo na urafiki katika mahusiano ya kimapenzi


Image result for makala za mahusiano

Watu Wengi Ambao Wako Kwenye Uhusiano Wanalalamika Kuwa Wenzi Wao Hawawaoneshi Upendo Kama Ilivyokuwa Siku Za Mwanzo Za Uhusiano Wao. Wanaeleza Kuwa Wanaona Uhusiano Wao Unalegalega Na Mapenzi Yanapungua Taratibu Kama Barafu Iyeyukavyo Juani.
Ili Kuepuka Yote Haya, Hauna Budi Kujifunza Njia Za Kuwasha Upya Moto Wa Upendo Kila Wakati Kwa Kuongeza Ukaribu (Intimacy) Kati Yako Na Mwenzako.
Zifuatazo Ni Mbinu Zitakazokusaidia
Kucheka Pamoja

Kicheko Ni Mlango Wa Ukaribu, Kama Mwaweza Kucheka Pamoja Basi Mwaweza Kulia Pamoja, Na Hapa Mwaweza Kuaminiana Zaidi Katika Kuwasiliana Hisia Zenu, Kama Waweza Kuitofuta Furaha Katika Kila Kitu Basi Unaweza Kupenya Katika Vyote. Usiwe Mgumu Na Mwenye Msimamo Mkali Katika Kila Kitu. Jifunze Kujizuia Pale Unapoanza Kuelekea Kwenye Kukasirika Na Badala Yake Tumia Kucheka Kama Mlango Wa Kutokea. Kama Utaanza Kujizoeza Hivi Ukiwa Nyumbani, Taratibu Utaweza Ukiwa Ofisini Na Hata Kwingine Kokote.
Kutiana Moyo

Kila Mmoja Awe Msaada Na Tegemeo Kwa Mwenzake. Jifunze Kumtia Moyo Na Kumwezesha Mwenzako. Sikiliza Na Kufuatilia Vile Mwenzako Afanyavyo Au Apendavyo.
Onyesha Heshima Katika Vitu Hivyo Pia. Kila Upatapo Nafasi Mpongeze Mbele Za Watu Au Hata Unapokua Nae Peke Yenu. Mjenge Mwenzako Mbele Ya wengine Na Kubali Pongezi Zote Za Mafanikio Yenu Zimwendee Yeye. Mruhusu Mpenzi Wako Ajue Kuwa Una Mkubali Katika Kila Afanyalo. Zaidi Tunavyo Wainua Wapenzi Wetu Ndivyo Wanavyotuthamini Na Kutunyanyua Na Sisi Pia.
Kupenda Kugusana

Nguvu Ya Mguso Wa Ukaribu Kamwe Haiwezi Kulinganishwa Na Chochote. Lazima Mjifunze Kujenga Tabia Ya Kugusana Mara Mpatapo Nafasi Sio Tu Mnapokuwa Mmelala. Kugusana Huku Ni Pamoja Na Kushikana Mkono Mkiongea Au Mkitembea, Kukumbatia Bega, Kugusa Au Kuchezea Nyewele Za Mwenzako Na Njia Nyingine Zozote Za Kuonyesha Ukaribu Kimwili. Wengi Wetu Huweza Kufanya Haya Kidogo Tunapokuwa Peke Yetu Na Kamwe Sio Mbele Ya Watu, Je, Ni Aibu, Nidhamu Mbaya? Dhambi?

Kugusana Ndiyo Mwanzo Wa Kuamsha Hisia Za Kuhitajiana, (Hebu Jiulize Kisirisiri, Lini Uligusana Na Mwenzako Nje Ya Chumba?). Kumgusa Umpendaye Hukuzuia Kutowaza Kumgusa Yeyote Katika Ulimwengu Uliojaa Wengi Walio Wapweke.

Mguso Huu Wa Upendo Haumaanishi Mguso Wa Tendo La Ndoa, Ingawa Pia Ni Vyema Kujifunza Kuijenga Lugha Ya Mguso Wa Tendo La Ndoa Katika Uhusiano Wenu.

Zungumza Hisia zako kwake
Kati Ya Vikwazo Vikubwa Katika Ustawi Wa Uhusiano Mengi Hususan Ya Wanandoa Ni Kutokuwepo Kwa Majadiliano. Lazima Wapenzi Wajifunze Kuzungumza Kuhusu Hisia Zao. Kama Vile Maisha Yasivyo Na Ukamilifu, Uhusiano Na Hata Ndoa Pia Hazina Ukamilifu. Mpenzi Wako Hayuko Kamili Na Wala Wewe Pia Siyo Mkamilifu. Jifunze Kuzungumza Na Umpendaye Jinsi Unavyojisikia Na Nini Kinachokusumbua. Kuendelea Na Migogoro Isiyosuluhishwa Husababisha Moyo Kuwa Baridi Juu Ya Mwenzako. Jiwekeeni Muda Kila Wiki Wa Kutoka Ili Kuzungumza Mambo Yenu. Mwambie Umpendaye Yapi Yanayojiri Kila Siku Na Zipi Ni Changamoto Zako Mkiweza Kujifunza Kuwekeza Katika Muda Wa Kuwa Pamoja Taratibu Hata Muda Wenu Wa Maongezi Ya Simu Utaongezeka.

Msamehe mpenzi wako na Kubali Kusamehewa naye
Kamwe Tusiache Maumivu Na Machungu Yatawale Uhusiano Wetu. Lazima Tujifunze Kuwasamehe Tuwapendao Na Kujisamehe Sisi Pia. Kutofautiana Katika Uhusiano Kupo Sana, Na Lazima Tuwape Tuwapendao Nafasi Ya Kuelezea Vile Vinavyowaudhi Dhidi Yetu. Kila Hisia Za Mmoja Wetu Zina Umuhimu. Huwezi Kujiona Vile Ulivyo, Mruhusu Mwenzako Akwambie Yanayomuumiza Na Msameheane.

Lina Muonekano wa Mpenzi wako
Mara Nyingi Hatari Hii Hutokea Tunapokuwa Katika Mizunguko Ya Huku Na Huko. Ukaribu Na Mpenzi Wako Hauendelezwi Tu Bali Unalindwa. Mwonekano Wetu Lazima Uwe Halisi Na Siyo Bandia . Vile Tunavyoviona Katika Tamthiliya Na Filamu Siyo Ukaribu Ulio Halisi. Kama Tunataka Tuonekane Sawa Na Vile Tunavyowaona Wengine Wanavyopendana Basi Tunakosea Na Kujizuia Kuwa Na Mtazamo Bora Katika Uhusiano Wetu. Ukianza Kupata Ukaribu Wa Kweli Baina Yako Na Mwenzako, Utapoteza Hisia Ya Kuhitaji Ukaribu Huo Na Mwingine Yeyote, Na Badala Yake Utaanza Kuulinda Ukaribu Mlionao.
Lengo Liwe Kuvitafuta Vile Vyote Mpenzi Wako Alivyonavyo Ambavyo Ni Kukuza Ukaribu Wenu. Mwenzako Awe Ndiyo Mtu Wa Muhimu Kuliko Wote Katika Maisha Yako.


FILAMU YA HAMISA MOBETO YAGEUKA GUMZO

Image result for hamisa mobeto photos

Filamu ya mwanamitindo Hamisa Mobeto iliyozinduliwa wiki iliyopita, katika hafla iliyofanyika katika ukumbi wa Suncrest Cineplex uliopo ndani ya Quality Center, uliopo Barabara ya Nyerere jijini Dar es Salaam, hivi sasa inatikisa jiji kwa kile kinachotajwa kuwa ina kiwango kikubwa cha ubora.
 
Kwa mujibu wa wadau waliozungumza na Risasi Mchanganyiko juzikati, filamu hiyo iitwayo Zero Player, imechukuliwa kwa viwango bora kabisa kuliko kazi nyingi zilizotolewa siku za hivi karibuni na zaidi ya hapo, pia hata waigizaji wake waliifanya kwa ubora wa hali ya juu.

Akizungumza na Risasi Mchanganyiko, mwanamitindo huyo ambaye alicheza filamu hiyo na wasanii wengine kutoka nchi mbalimbali zikiwemo  Afrika Kusini, Ghana, Cameroon, Nigeria na Tanzania na pia filamu hiyo imerekodiwa katika kiwango kizuri sana na kila mmoja amecheza inavyopaswa katika nafasi yake.

“Kwa kweli ni filamu ambayo nimecheza lakini hata mimi mwenyewe naifurahia jinsi nilivyoitendea haki nafasi yangu, imenionyersha kiasi gani nimekua katika tasnia hii,” alisema Mobetto, mama wa watoto wawili. Baadhi ya wasanii walioudhuria uzinduzi huo walipongeza filamu hiyo na kusema kuwa imechezwa katika kiwango kizuri sana na chenye ubora wa uhakika huku wakiwapongeza wasanii ambao wamecheza filamu hiyo.

“ Yaani kiukweli nimeangalia filamu hii nimependa sana jinsi walivyocheza wameonekana wako makini na wanajua ni kitu gani wanakifanya katika uigizaji huo na pia wameweza kuwafunika hata wakongwe” alisema Ester Kiama

Wanawake wenye ulemavu wa ngozi kuandika historia mpya kwa kupanda mlima Kilimanjaro.   Mwanaharakati wa haki za binadamu na mp...