Ijumaa, Machi 02, 2018

Wanawake wenye ulemavu wa ngozi kuandika historia mpya kwa kupanda mlima Kilimanjaro.

 
Mwanaharakati wa haki za binadamu na mpigania mabadiliko Jane Waithera akishirikiana Na mshindi wa tuzo ya muandaaji wa filamu na mpandaji wa milima mbalimbali Elia Saikaly wameandaa mradi unaojulikana kama "climb for Albinism"(kwea kwa ajili ya ualbino) ambapo wanawake sita kutoka Afrika wamejipanga kukwea mlima Kilimanjaro wenye kilele kirefu zaidi kuliko yote barani Afrika.

Akiongea na waandishi wa habari jana jijini Dar es salaam muanzilishi wa programu hiyo Elia Saikaly amesema kuwa Mara nyingi watu wenye ualbino wanaonekana kama waathirika na kusema kuwa wana mpango wa kuvunja dhana hiyo kwa kufanya kitu ambacho hakijawahi kufanyika na kusistiza kuwa wataionyesha dunia kwamba licha ya changamoto nyingi zinazowakabili na kusema kuwa wanawake hao wana nguvu, wana uwezo na ni mfano wa kuigwa kwa wanawake wengine duniani.

Aidha kiongozi mwenza wa "climb for albinism" Jane Waithera amesema kuwa watakaposimama kweye kilele cha Afrika, timu nzima itatuma ujumbe madhubuti utakaosaidia kuelimisha jamii na kuondoa mitizamo hasi inayoeneza fikra mbaya kuhusu watu wenye ualbino.

Kwa upande wake kiongozi wa shirika la under the same sun Peter Ash linalotetea haki na usitawi wa watu wenye ualbino kwa kuelimisha jamii kuhusu ualbino , amesema kuwa wanaunga mkono shughuli hizo za kupanda mlima huku akisisitiza kuwa wana ndoto kwamba siku moja watu wenye ualbino watachukua nafasi yao inayostahili kwenye jamii na kwamba siku za ubaguzi dhidi ya watu wenye albino zitakuwa kumbukumbu iliyofifia na kusema kuwa upandaji wa mlima huu utaionesha duniani kwamba ndoto hii inaweza kutimia.

Pia Nodumo Ncomanzi ambaye ni moja kati ya wapanda milima kutoka Zimbabwe amesema kuwa kupanda mlima ni njia nzuri itakayoonesha na kuwakumbusha watu kwamba albino Wapo na wanajitegemea na wanawake wenye ualbino wanastahili kupewa fursa ya kukabiliana na kuzishinda changamoto mbalimbali zinazowakabili.

RC MAKONDA AFANIKISHA NDOTO YA AHMED ALBAITY






Ndoto na shauku ya kijana Ahmed Albaity alieteseka kwa zaidi ya Miaka 10 Kitandani kwa kushindwa kumudu gharama za matibabu leo imebadilika kuwa furaha baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda kumkabidhi  Tiketi za Ndege za watu Wanne kwaajili ya safari ya kwenda kupatiwa matibabu Nchini China kwenye Hospital ya Beijing Puhua International huku akijitolea pia kugharamia fedha za Matibabu na Malazi.

 Makonda alitoa ahadi kumsaidia Ahmed Albaity wakati wa Zoezi la Upimaji Afya Bure kwenye Meli ya Jeshi la China mwishoni mwa Mwaka Jana baada ya kugundulika Ahmed anahitaji Matibabu Maalum ambayo hayapatikani kokote kule duniani isipokuwa China, jambo lililomfanya RC Makonda kutokwa na Machozi na Kuhaidi Kumpeleka kwenye matibabu kwa gharama yoyote ile *Maumivu na Mateso* anayopitia kijana huyo.

Ahmed Albaity anasumbuliwa na tatizo la uti wa mgongo baada ya kuanguka na kuvunjika Shingo alipokuwa akiogelea ambapo kwa sindano moja pekee inagharimu Dollars 26,000/= sawa na shillingi million 52.

RC Makonda amesema Ahmed atasafiri Nchini China Siku ya Jumapili akiongozana na watu watatu wa kumsaidia kumuhudumia ambapo gharama zake ni zaidi ya Shilingi Million 100.

Aidha RC Makonda amesema Shauku yake ni kugusa maisha ya Mwananchi hata kama ni mmoja atakaekwenda mbele za Mungu na kusema Asante Mungu kwa kutupatia viongozi wetu, ifike mahali tumtumikie Mungu katika nafasi zetu, na katika hilo watu wote watakuwa Sawa na tutawahudumia bila kutarajia chochote kutoka kwao kama sehemu ya utumishi wetu ambapo amewashukuru watu wote waliomchangia na kufanikisha matibabu.

Hata hivyo RC Makonda ametoa wito kwa wananchi wa dini zote kumuombea Ahmed ili aweze kupona na kuendelea na shughuli za ujenzi wa Taifa.

Kwa upande wa Ahmed Albaity amemshukuru RC Makonda kwa moyo wa ukarimu aliouonyesha ambapo ameeleza kuwa ameishi kwa mateso muda mrefu kutokana na kukosa uwezo wa kumudu gharama za matibabu.

Aidha amesema alipokuwa akiomba watu wamchangie wapo waliokuwa wakimvunja moyo kwa kumwambia hawezi kupona lakini RC Makonda ameonyesha moyo wa kipekee.

Jumatano, Januari 10, 2018

Yanga Leo kukipiga na URA




KIKOSI cha Yanga, leo kitapambana na URA ya Uganda katika mchezo wa nusu fainali ya michuano ya Mapinduzi inayoendelea kutimua vumbi mjini Unguja huku kocha wa Simba akiwapa mbinu. Mechi hiyo inayotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa itafanyika kwenye Uwanja wa Amaan mjini Unguja.


Hata hivyo, Aliyekuwa Kocha Mkuu wa Simba, Mcameroon, Joseph Omog ambaye hivi karibuni alifungashiwa virago na klabu hiyo, ameitaka Yanga kuhakikisha inacheza kwa nidhamu kubwa na URA kama inataka kuibuka na ushindi.

Akizungumza kwa njia ya simu kutoka kwao Cameroon, Omog alisema, kuwa wachezaji wa URA wanacheza kwa nidhamu kubwa na kwa ushirikiano wa hali ya juu ndiyo maana katika michuano hiyo timu hiyo inaonekana kuwa ni ngumu.

Alisema wachezaji wa Simba walipoteza umakini katika mechi zao na kushindwa kuzitumia vizuri nafasi walizokuwa wakizipata jambo ambalo ndilo limesababisha washindwe kuibuka na ushindi katika michezo yake. Amesema kwenye mechi dhidi ya URA walipoteza umakini ndiyo maana walifungwa kirahisi.

“Nimesikitishwa na kitendo cha Simba kuondolewa katika michuano hiyo lakini kila mtu anapaswa kukubaliana na matokeo hayo na hivyo ndivyo mchezo wa soka ulivyo. “Wachezaji wa Simba walipoteza kidogo umakini katika mechi hiyo ambayo video yake nimeiona leo (jana) kupitia mtandao baada ya kutumiwa na rafiki yangu mmoja ndiyo maana walifungwa japokuwa walicheza vizuri.

“Kwa hiyo, Yanga wanatakiwa nao kuwa makini katika mechi hiyo, kila mchezaji aingie uwanjani kupambana na kuyafanya majukumu yake kwa ufanisi mkubwa kama kweli wanataka kuibuka na ushindi, nimewaona URA ni wazuri na wanacheza kwa akili sana. “Yanga watafanya kosa kama watawaachia nafasi ya kutawala mchezo huo,” alisema Omog ambaye mwaka jana aliongoza timu hiyo kutinga fainali ya michuano hiyo lakini ikifungwa na Azam FC

Baada ya Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Lowassa kumtembelea Rais Magufuli...Mbowe azungumza haya

Baada ya Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Edward Lowassa kumtembelea Rais John Magufuli Ikulu jijini Dar es Salaam na kufanya nae mazungumzo, Mwenyekiti wa Chama hicho, Freeman Mbowe amesema kuwa kile kilichosemwa na Lowassa  sio msimamo wa CHADEMA bali ni mawazo yake binafsi.

Akizungumza jana na Idhaa ya Kiswahili ya Shirika la Utangazaji BBC, Mbowe alisema wao kama Chama wamekuwa na utaratibu wa kutoa msimamo wao na kueleza kuwa kwa siku za hivi karibuni wamekuwa na malalamiko dhidi ya Rais na Serikali yake kuhusu kuminywa kwa Uhuru wa Bunge, Mahakama na kuminya Demokrasia.

" Tunaona jinsi ambavyo uhuru wa watu unaminywa, uhuru wa vyombo vya habari, wandishi, wanasiasa na wananchi kutekwa, kudorora kwa uchumi, unaanzaje kumuunga mkono Rais nafikiri muhusika aulizwe mwenyewe," alisema Mbowe.

Kuhusu kauli ya Lowassa kusifia ongezeko la ajira, Mbowe anasema hayupo tayari kujibu hoja hiyo lakini akaeleza namna ambavyo makampuni mengi yanafungwa hivi sasa, kundi kubwa la vijana wasio na ajira likiwa mitaani.

" Nisikitike tu kuwa sisi tuna tatizo kubwa sana la kumuuguza Lissu ambaye alipigwa na risasi, kweli anaweza kutoka kiongozi mkubwa na kumsifia Magufuli wakati tunauguza watu? 

"Msaidizi wangu Ben Saanane amepotea hadi leo, wabunge wetu wanafukuzwa bungeni hivyo niseme tu hakuna msimamo kama huo ndani ya Chama labda atafutwe muhusika mwenyewe aeleze," Alisema Mbowe.

Akizungumzia hama hama kwa wabunge na wanachama wa upinzani na kujiunga na CCM sambamba na tukio la jana  la Mjumbe wa Kamati kuu ya Chama hicho, Muslim Hassanal kujiunga na CCM , Mbowe alisema suala la wapinzani kuhamia CCM halijaanza leo na kwamba suala la kujenga upinzani ulio imara lazima lipitie hatua mbalimbali ili kufanya mchujo wa kubakia na watu wenye dhamira ya kweli

Wanawake wenye ulemavu wa ngozi kuandika historia mpya kwa kupanda mlima Kilimanjaro.   Mwanaharakati wa haki za binadamu na mp...