Ijumaa, Agosti 25, 2017

MAKONDA 'KERO YA KUKOSEKANA KWA MAJI JIJI LA DAR ES SALAAM SASA KWISHA KABISAA!!!'

Meneja uendeshaji wa mradi Mhandisi Lydia Ndibaleme akimuonesha Mkuu wa Mkoa Paul Makonda mchoro wa ramani wa mradi huo utakao jengwa katika eneo la Jangwani Jijini Dar es salaam

SERIKALI mkoani Dar es Salaam, imetangaza kujenga miradi  mitatu mikubwa   ya maji  itayo maliza tatizo la uhaba wa maji jijini humo.

MKUU wa Mkoa wa  Dar es Salaam, Paul Maonda,  ametembelea  miradi  mbalimbali  inayosimamiwa na Mamlaka  la Maji safi na Majitaka  mkoani Dar es Salaam (DAWASA).

Miradi hiyo ni  pamoja na ile ya uondoaji  na usafishaji wa majitaka, miradi wa uboreshaji  huduma za usambazaji  maji katika  baadhi ya maeneo  ya Mkoa wa Pwani na Dar es Salaam.

Pia miradi ya uchimbaji wa  visima  katika wilaya ya Ubungo.

Lengo la ziara hiyo ilikuwa  kukagua maendeleo ya shuughuli mbalimbali za ujenzi wa miradi  mipya iliyo na lengo la  kumaliza tatizo la majisafi  na maji taka katika  jiiji la Dar es Slaam.

Huu ni muendelezo wa ziara zake alizo  anza hivi karibuni  ambapo tayari ametembelea chanzo kipya cha maji Kimbiji wilayani Kigamboni  ambako kuna miradi ya uchimbaji  wa visima virefu vyenye urefu wa kina cha mita 600 na miradi iliyokamilika  ya upanuzi  wa mitambo ya   Ruvu Juu na Chini mkoani Pwani.

Mradi wa ujenzi wa mitambo mitatu mikubwa  na ya kisasa ya kusafisha majitaka itakayo kwenda sabamba na ulazaji maboomba ya ukusanyji  maji taka itajengwa katika eneo la Jangwani, Mbezi beach  na Kurasini ili kuongeza kiwango cha` kusafisha  majitaa  cha asilimia 10  cha sasa kufikiaa asilimia 30 ifikapo mwaa 2020.
Mafundi wakiendelea na ujenzi wa mradi tenki la maji eneo la Mabwepande Dsm
Gharma za  jumlaza miradi hii ni  dola milioni 600.

Miradi hii  inatekelezwa  kwa awamu tatu,  na awamu ya kwanza  inaanza ndani  ya mwaka huu wa fedha 2017/18.

Mradi wa mfumo wa majitaka  jangwani  unahusu  ujenzi wa mtambo wa kusafishia majitaka   ambapo ukapokamilika  utakuwa  n uwezo wa  kusfisha mta za ujazo 200,000 kwa siku.

Mfumo wa mabomba yenye  urefu wa kilomita 376 yatakay9lazwa kuanzia Ubungo hadi Jangwani, Kinondoni, Mwananyamala mdsasani  na katikati ya jiji utajengwa.
Afisa mtendaji mkuu wa Dawasco Cyprian Luhemeja (Kulia) akimuelezea Mkuu wa mkoa Paul Makonda namna mradi huo utakavyomaliza tattizo la maji Jijini Dar es salaam endapo utakamilika
Awamu ya kwanza ya ujenzi itahusisha sehemu  itakayoweza kusafisha mita  2500 kwa siku  na mabomba ya kilomit 17.43 yataakayojengwa katikaa eneo la magomeni.

Pia katika awamu ya kwanza  bomba linalomwaga majitakaa  baharini litaacha kutumika na badala yake majitaka hayo yatasafishwa  kwa kutumia mtambo huo.

Mtambo huo unajengwa kwa ushirikiano wa serikali ya Tanzania na  korea kupitia mkopo  wa  masharti nafuu  kutoka benki ya exim ya korea.

Unatarajiwa kugharimu  dola za marekani milioni 90. Taratibu  za ununuzi  zinaeendelea  ili  kumpata  mshauri  na hatimye mkandarasi  lengo likiwa ni kuanza ujenzi mapema mwaka 2018.
Mfumo  wa majitaka mbezi  utjengwa  kilongwima  na utakuwa na uwezo wa  wa ,kusafisha  mita za ujazo 16000 kwas iku . utajengwa na serikali ya Tanzania  kwa kushirikiana na  benki ya dunia kupitia mkopo  wa masharti nafuu na unatarajiwa kugharimu  dola milioni 65.

Ujenzi  wa mtambo wa kusafisha maajitaka kurasinini utakuwa na mfumo wenye urefu wa kilomita  90 utakaolazwa katia maeneo ya changombe , kurasini, temeke  na uwanja wa taifa.

Mradi huo utajengwa kwa kushirkiana  na  shirika la maendeleo la ufaransa  afd na utakuwa na uwezo wa kusafisha  mita za ujazo  11,0000 kwa siku.

Mitambo hiyo  itawezesha   kuzaisha gesi asilia  na umeme kwaajili ya kuendeshea  mkitambo  hiyo hivyo kupunguza  matumizi ya gharama za umeme na vilevile  maji yatakayokuwa  yametbiwa  yatauzwa  na kutumika katika shughuli mbalimbali  kama ile  kupoozea mitambo na umwagiliaji.

Tope litakaobakibaada ya mchkato huo  wa usafishaji majitaka  litaweza utmika kama mbolea  kwaajili ya  kilimo panja  na bustani za majani na miti ya kivuli na hivyo kupendezesha jiji.

Pamoja na miradi hiyo  mradi mwingine ni wa uboreshaji  mfumo wa usambazaji maji  ambao  unahusisha ujenzi wa matenki tisa ya kuhifadhia maji na kusambaza  maji yenhye ukubwa wa kuhifadhi  lita za ujazo milioni  tatu hadi milioni aita.

Meneja uendeshaji wa mradi Injinia Lydia Ndibaleme akizungumza na Waandishi wa habari katika ziara hiyo jinsi ambavyo wata utekeleza mradi huo namna ambavyo wananchi watanufaika kwa kiasi kubwa Pwani na Jijini Dar es salaam.

Pia ujenzi wa vituo  vine  vya kusukum maji, ununuzi  wa transifoma,  na ufungaji  njia za umeme   wa msongo wa  mkubwa   na ulazaji mabomba  makubwa  ya ugawaji  maji   na mabomba ya  usambazaji  maji yataayokuwa na urefu wa kilomomita 477.

Maeneo yanayotarajiwa kunufaika  na mradi huo  ni changanyikeni, bagamoyo,mpiji, zinga , kiromo , kitopeni  ukumi kerege buma mataya na ukanda maalumu ya eoz 

Lengo la mradi huu ni kuhakikisha wananchi wote  wa kawaida  wenye viwanda  na bashara katika eneo  lote la mradi wanapat huduma bora za maji hasa baada ya maji kuongezeka  kufuatia kukamilika kwa kazi zaupanuzi wa mitamb ya maji ya ruvu juu na ruvu chini.

Mradi huo utgharimu  dola za marekani milioni32 kupitia mkopo wa masharti nafuu kutoka serikali ya inda.

Pia  mradi wa uchimbaji wa visima katika manispaa ya ubungo  ili kuwapunguza changamoto wakati miradi mikubwa ya usambazaji  maji ikisubiriwa kutekelezwa.

Mkataba ulisainiwa aprili  11,2017 na unatarajiwa  kuisha agosti 31, 2017  mbapo visima 10 viatarajiwa kkuchimbwa   ambapo utagharimu   shilingi milioni109.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Wanawake wenye ulemavu wa ngozi kuandika historia mpya kwa kupanda mlima Kilimanjaro.   Mwanaharakati wa haki za binadamu na mp...